Friday, 1 April 2016

MBUNGE WA MANONGA AMETOA MSAADA WA VIFAA VYA MICHEZO

Mashindano ya UMISETA NA UMITASHUMITA nchini yakitazamiwa kuanza  hivi karibuni kitaifa, kiwilaya na kimkoa, Mbunge wa jimbo la Manonga (Igunga Tabora) Seif Khamis Gulamali, ametoa vifaa vya michezo katika shule za sekondari na shule za msingi katika jimbo lake
Pichani; Wa kwanza kulia Mbunge wa Manonga Seif Khamis Gulamali akiwa katika pozi na
moja ya wachezaji wa timu ya Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania (Picha na Maktaba)

Mbunge huyo ametoa vifaahivyo vya michezo katika Shule 13 za Sekondari na Shule za Msingi karibu 50 za Jimbo la Manonga.
"Kwa kuanzia Tumezipatia Vifaa vya Michezo kama Mipira ya Footballs, Netballs, Basketballs, Handballs na Volleyballs,"Jumla ya Mipira 180 tumegawa nikiwa kama Mbunge wa Jimbo la Manonga ikiwa na lengo la kukuza na kuboresha sekta ya Michezo Jimboni". Amesema Mh. Seif Khamis Gulamali
Mh Gulamali amesema hii itapelekea kukuza Viwango vya wanamichezo katika jimbo la Manonga na wilaya ya Igunga kwa ujumla ndio maana ametoa vifaa hivyo

UPANUZI WA MASAFA YA USIKIVU WA TBC,KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII YATEMBELEA KISARAWE

tib1
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akisalimiana na mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya bunge ya huduma na maendeleo ya jamii Bw.Peter Serukamba katika viwanja vya urushaji wa matangazo ya shirika la utangazaji Tanzania (TBC) Kisarawe
tib2
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na maendeleo ya Jamii Bw.Peter Serukamba akieleza jambo wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kuangalia mradi wa upanuzi wa masafa ya usikivu ya shirika la utangazaji Tanzania iliyopo kisarawe Pwani.
tib3
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye (wa pili kulia) akiwasilisha jambo kwa wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na Maendeleo ya jamii walipotembelea mradi wa upanuzi wa masafa ya usikivu ya shirika la utangazaji Tanzania iliyopo kisarawe Pwani.
tib4
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na maendeleo ya Jamii Bw.Peter Serukamba akieleza jambo wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kuangalia mradi wa upanuzi wa masafa ya usikivu ya shirika la utangazaji Tanzania iliyopo kisarawe Pwani.
tib5
Mkurugenzi wa shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Bw.Ayoub Ryoba akiwasilisha  taarifa ya shirika hilo  kwa wajumbe wa wa kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na Maendeleo ya jamii kuhusiana na upanuzi wa masafa ya usikivu kisarawe Pwani.Wengine pichani ni Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye,Naibu Waziri wa wizara hiyo Bi.Anastazia Wambura na mwenyekiti wa kamati hiyo Bw.Peter Serukamba
Picha na Daudi Manongi-Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Tuesday, 21 October 2014

MBELE YAKE NYUMA YETU BURIANI YP


Msanii 'YP' toka kundi la TMK Wanaume Family amefariki dunia jana usiku katika hospitali ya Temeke ambako alikuwa akipatiwa matibabu akisumbiliwa na kifua kwa muda mrefu lakini hali ilikuwa mbaya katika wiki mbili kabla ya kifo chake. 

pichani YP enzi za uhai wake

Meneja wa TMK Wanaume Family na mkubwa na wanawe Said Fela amethibitisha kutokea kwa msiba huo. Msiba wa msanii huyo uko Keko nyumbani kwa baba yake.

Said Fella amesema Marehemu ambaye jina lake halisi ni Yessaya Ambikile alifanya vizuri na msanii mwingine Y Dash na nyimbo kama 'Ulipenda Pesa', 'Pumzika', 'Shemsha' na nyimbo nyingi za TMK Wanaume Family kama 'Twende zetu' ya Chege, 'Dar mpaka Moro', 'Kichwa kinauma', 'Tufurahi' na nyimbo nyingi za TMK Wanaume family

Monday, 22 September 2014

MH. KINANA AWATAKA WANANCHI BAGAMOYO KUJIUNGA NA MIFUKO YA AFYA YA JAMII


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwapungia mkono wakazi wa Bagamoyo wakati wakiwasili kwenye uwanja wa mkutano wa shule ya Msingi Jitegemee.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimpa mkono wa pongezi mshahiri maarufu wa CCM mkoa wa Pwani Ndugu Ali Pongwe baada ya kutoa ushairi mzuri kabla ya kuanza kwa mkutano.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kata ya Magomeni wilaya ya Bagamoyo ambapo aliwasisitiza kujiunga na mfuko wa afya ya jamii pamoja na wazazi kuwapeleka watoto shule pia aliwashauri wazazi kuchagua watu wenye shughuli zao kuingia kwenye kamati za shule kwani kutasaidia sana kupunguza michango isiyo ya lazima.
 Wananchi wa kata ya Magomeni wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mheshimiwa Mwantumu Mahiza akihutubia wakazi wa kata ya Magomeni na kuwataka kuhakikisha watoto watakaochaguliwa kuingia sekondari wanaenda shule kwani kushindwa kufanya hivyo ni kurudisha nyuma maendeleo.Pia aliwataka wananchi wachunge afya zao kwani elimu ya maambukizi ya ukimwi inatolewa ya kutosha hivyo kila mtu anapaswa kuwa makini na afya yake.
 Sehemu ya watu waliohudhuria mkutano.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kata ya Magomeni ambapo alitoa sifa kwa Mkuu wa mkoa wa Pwani kwa utendaji wake wenye ufanisi mkubwa pia aliwaambia wananchi hao kuwa vyama vya siasa ndio vimeshafika muda wake kwani havina sera na vimeshindwa kuja na sera mbadala ya kuleta maendeleo ya kiuchumi nchini.
 Wananchi wakimsikiliza Nape Nnauye ambaye pia aliwataka watendaji wa Serikali kuwa karibu na wananchi kwani kutasaidia kufanikisha maendeleo na kuondoa sintofahamu za wananchi wanaotaka kujua taarifa za maendeleo ya miradi au maeneo husika.
Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Dk.Shukuru Kawambwa akihutubia wakazi wa jimbo lake wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Jitegemee ambapo aliwaambia kero za michango midogo midogo zinaondolewa .
 Katibu wa CCM mkoa wa Pwani Joyce Masunga akihutubia wakazi wa kata ya Magomeni ambapo aliwaambia  wanawake kutokuwa nyuma katika kuomba nafasi za uongozi katika chaguzi zinazokuja.
 Mmoja wa wananchi waliofika kwenye mkutano akiuliza swali kwa Katibu Mkuu wa CCM wakati wa mkutano .

 Diwani wa kata ya Magomeni Bi.Mwanaharusi Jarufu akijibu moja ya maswali yaliotoka kwa wananchi.
 Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo akijibu maswali kutoka kwa wananchi
Sehemu ya wanachama wapya waliopokea kadi zao za uanachama leo mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ambapo zaidi ya wanachama 338 walijiunga na CCM

Tuesday, 26 August 2014

MABINGWA MARA MBILI MFULULIZO WA KOMBE LA TASWA WAPIGWA MVUA YA MABAO LEO



MABINGWA MARA MBILI MFULULIZO WA KOMBE LA      TASWA WAPIGWA MVUA YA MABAO LEO

Mabingwa wa kombe la taswa kanda ya kaskazini ambao ni chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha (AJTC) wamemiminiwa mvua ya magoli matatu kwa mbili na timu ya SOMBETINI PARISH FC mapema leo.

 Mtanange huo ambao umepigwa mida ya saa kumi za jioni katika viwanja vya FFU Arusha umezikutanisha timu hizo mbili katika robo fainali ya kombe la NANI ZAIDI lililojumuisha timu kama AJtC stars,Sombetini Parish fc,FFU na zingine kibao.
Ikiwa na mchezo wa sita kwa kila timu Sombetini Parish imejiwekea rekodi ya kutofungwa mechi hata moja katika ligi hii wakiwa wameibuka na ushindi wa michezo mitatu na suluhu katika michezo mitatu waliyoweza kucheza.

Na timu ya Ajtc stars imeweza kushinda michezo mitatu,sare mchezo mmoja  na kuchabangwa katika michezo miwili waliyoweza kucheza katika ligi hii,matokeo yamchezo wa leo umeitoa timu ya Ajtc stars katika mashindano na kuiruhusu Sombetini parish kuingia katika nusu fainali ya ligi hii.
Mabao katika mchezo huo,Ajtc stars ilianza kwa kutupia goli kupitia mpira wa adhabu uliopigwa na mshambuliaji wa timu hiyo Fred ’16 dakika ya tatu ya mchezo huo ambae pia alirudi golini na kutupia bao la pili katika dakika ya tisini ya mchezo.

Pichani ni baadhi ya wachezaji wa Ajtc stars
 Kwa upande wa washindi wa mchezo huo Sombetini Parish  mabao yaliwekwa kimyani na Emmanuel ’11 katika dakika arobaini ya mchezo,bao la pili kupitia nahodha wa timu hiyo Sam Petro dakika arobaini na tano ya mchezo na kapu la  mabao lilihitimishwa na Frank Ally kupitia mkwaju wa penati dakika ya sabini ya mchezo.

(Pichani) Kocha wa AJTC stars bwana Idrissa Bakari akiongea na wanahabari uwanjani Field force leo



 Mchezo huo ambao timu hizo zilionyesha kukamiana na kila mmoja kutaka kulichungulia lango la mwenzie ila Sombetini iliibuka kidedea kwa mabao 3-2 dhidi ya Ajtc stars.
Akizungumza na IGUNGA NEWS kocha wa timu ya Ajtc stars amesema huo ni moja ya mchezo sababu kuna kushinda,kushindwa na suluhu na kupoteza mchezo wa leo ni changamoto kwake,Pia akaongezea kusema japo watu wanamlaumu kuchezesha mamluki katika kikosi chake akasema hayo ni maneno ya mashabiki tu. 

           “unajua kushindwa,kushinda na suluhu ni moja ya mchezo na kupoteza mchezo wa leo ni changamoto kwangu na siwezi kuwa ‘’BLAME’’ wachezaji wangu wameshindwa kutengeneza ‘’chemistry’’ ya mchezo na nahitajika kujipanga kwa michuano mingine kuhusu mamluki hao ni mashabiki tu wanaongea hivyo”,alisema kocha Idrissa Bakari

Pichani Mwenye suti nyeusi Kocha wa Sombetini bwana Kamanda akitoa ufafanuzi juu ya mchezo wa leo kwa waandishi wa habari leo
Nae kocha wa Sombetini Parish amesema ushindi huu ulikuwa ni wa lazima kwao kutokana na maandalizi ya michuano hiyo waliyoyafanya kuanzia mwanzo na wamejipanga vizuri katika kuingia katika nusu fainali ya michuano hiyo na amelaumu kwa wachezaji wake kupewa kadi zisizo za lazima.

         ‘’Yaa ushindi wa leo ulikua ni wa lazima kwetukutokana na maandalizi katika mashindano haya tuliyoyafanya tokea mwanzo na tumejipanga vizuri kwa kufanya mazoezi na leo tumepewa kadi zisizo za lazima ila si kwamba timu haina nidhamu’’,alisema kocha Kamanda.

Pichani mashabiki wa Sombetini Parish wakisherehekea ushindi dhidi ya Ajtc stars
 Ushindi wa leo umewapa nafasi Sombetini Parish kuwa na mchezo siku ya ijumaa na wanasema wamejipanga vyema katika kuingia kwenye mchezo huo na kuahidi ushindi kwa timu hiyo.
Pia IGUNGA NEWS iliweza kuongea na mashabiki wa timu zote mbili na kusema timu zo zimecheza vilivyo na matokeo yaliyotokea ni moja ya mchezo na wameahidi kuendelea kuzishabikia timu zao.  

Friday, 15 August 2014